Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Eisleben

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jumba lamanisipaa nakanisa kuu la Eisleben
Martin Luther alifariki katika nyumba hii

Eisleben nimji katikajimbo laSaksonia-Anhalt nchiniUjerumani. Mji huu ni mashuhuri kama mahali pa kuzaliwa kwaMartin Luther na kwa hiyojina rasmi niLutherstadt Eisleben (Eisleben Mji wa Luther). Mnamomwaka2015 Eisleben ilikuwa na wakazi 24,198.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Mji huu mdogo una historia ndefu. Ilitajwa mara za kwanza katika hati ya mwaka994BK.

Katika karne ya 12 ulikuwa mji mkuu wa dola dogo la makabaila wa Mansfeld. Dola hili pamoja na mji wa Eisleben lilitajirika katika karne ya 13 baada ya kugunduliwa matapo yashaba na kuanzishwa kwa migodi ya kuchimba madini haya na tasnia ya kuyeyusha shaba hapa.

Katika karne ya 18 eneo la Mansfeld ilikuwa sehemu ya milki yaSaksonia na baadaye yaPrussia. Baada ya ugawaji wa Prussia mwaka 1945 mji ulikuwa sehemu ya jimbo la Saksonia-Anhalt.

Eisleben si mji tu wa kuzaliwa kwa Luther ni pia mahali alipohubiri mara ya mwisho wa kifo na kuaga dunia. Nyumba za kuzaliwa na kufa kwake ni mahali pa makumbusho zilizopokelewa katika orodha yaurithi wa dunia yaUNESCO.

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo yaUjerumani bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuEisleben kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Eisleben&oldid=1150587"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp