Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Dublin

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jiji la Dublin
Majiranukta:53°19′48″N6°15′0″W /53.33000°N 6.25000°W /53.33000; -6.25000
NchiEire
MkoaLeinster
WilayaDublin
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla505,739
Tovuti:  www.dublincity.ie

Dublin (Kieire pia:Baile Átha Cliath = "Kijiji kwenye kivuko kwa mafunjo") nimji mkuu waJamhuri ya Eire pia mji mkuu kwenye kisiwa cha Eire mwenye wakazi milioni 1.6 kwenye rundiko la jiji.

Jiografia

[hariri |hariri chanzo]
Poa kabisa: hali ya hewa ya Dublin

Dublin iko kando la mdomo wamto Liffey unapoishia katikaAtlantiki kwenye pwani la mashariki la Eire.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Wataalamu kadhaa hujaribu kuona uhusiano kati ya mji wa "Ebalana" uliotajwa na katika maandiko yaPtolemeo mnamo 140 BK lakini hakuna uhakika kuhusu mahali pake.

Mji wa leo ulianzishwa kama kiji cha wavuvi kwa jina la „Áth Cliath“ na kando lake Wavikingi walijenga kijiji cha jirani cha „Dubh Linn“ ("matope mweusi"). Vijiji vikaungana na kuwa mji tangu 1172 kwa sababuWanormandi baada ya kuvamia Eire kutoka Uingereza walianzisha makao makuu yao hapa. Katika kipindi hadi karne ya 16 Dublin ilikuwa kitovu cha eneo lililokuwa chini ya wafalme wa Uingereza kisiwani na tangu 1541 mji mkuu wa Ufalme wa Eire uliotawaliwa na mfalme wa Uingereza.

Baada ya muungano wa Uingereza na Eire katikaUfalme wa Muungano Dublin ilikuwa makao ya gavana mwingereza.

Uhuru wa Eire ulianza1916 mjini Dublin kwenye uasi wa Pasaka. KwenyeVita ya Uhuru ya Eire nyumba nyingi ziliharibiwa.Tangu uhuru wa 1922 Dublin ikawa mji mkuu.

Baada ya kujiunga kwa Eire na Umoja wa Ulaya Dublin imeendelea kukua na kuwa jiji ya Kiulaya. 1998 Dublin ilisheherekea sikukuu ya kumaliza miaka 1000.

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Picha za Dublin

[hariri |hariri chanzo]
  • Kanisa Kuu la Kristo Mfalme
    Kanisa Kuu la Kristo Mfalme
  • Manisipaa ya Dublin
    Manisipaa ya Dublin
  • Nyumba ya forodha
    Nyumba ya forodha
  • Mnara wa Boma la Dublin
    Mnara wa Boma la Dublin
Makala hii kuhusu maeneo yaIreland bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuDublin kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Dublin&oldid=1336284"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp