Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Dola Takatifu la Kiroma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Dola Takatifu la Kiroma si sawa naDola la Roma la Kale.
Ramani ya Dola Takatifu la Kiroma yaonyesha mikoa yake.
Maeneo ya Dola Takatifu la Kiroma pamoja na mipaka ya nchi za sasa.

Dola Takatifu la Kiroma (Kijerumani:Heiliges Römisches Reich,Kilatini:Sacrum Romanum Imperium) lilikuwa jina laUjerumani kati ya takriban mwaka1000 na1806. Lakini dola hilo, licha ya Ujerumani, lilikuwa pia na maeneo makubwa, yakiwa ni pamoja naAustria,Italia ya Kaskazini,Ubelgiji,Uholanzi naUcheki wa leo.

Mipaka yake yalibadilika mara kadhaa katikakarne nyingi za kuwako kwake.

Tabia za Dola

[hariri |hariri chanzo]

Maeneo hayo yote yaliunganishwa chini yaKaisari aliyekuwa pia mfalme wa Wajerumani.

Maeneo hayo yalikuwa na kiwango kikubwa cha kujitegemea yakitawaliwa na makabaila wa ngazi mbalimbali na maaskofu waKanisa Katoliki au yakiwa miji huru.

Halikuwa dola la kisasa, kwa kuwavyombo vya dola vilikuwa vichache. Kaisari alitegemea hasa mali yake binafsi pamoja na haki ya kuthibitisha watu waliopokea vyeo mbalimbali.

Tangu1438 hadi1806 cheo cha Kaisari kilibaki katika familia yaHabsburg waliotawalaAustria.

Chanzo baada ya Karolo Mkuu

[hariri |hariri chanzo]

Asili ya dola lilikuwa milki yaKarolo Mkuu aliyefaulu kuunganisha Ujerumani,Ufaransa na Italia chini yake. Mwaka800 alipokea cheo cha Kaisari wa Roma kutoka mikono yaPapa Leo III.

Hatua hii ilichukuliwa kama kuendelezwa kwa Dola la Roma la Kale katika magharibi ya Ulaya hata kama hali halisi ilikuwa kwamba milki ya Karolo ilikuwa milki yaWafranki naWagermanik wengine na taasisi zote zaRoma ya Kale zilikuwa zimeshakwisha kabisa katika magharibi ya Ulaya.

Yaliyobaki ya Roma ya Kale yaliendeleaUlaya mashariki kwa umbo laMilki ya Bizanti.

Lakini makaisari walijenga hoja la "translatio imperii" (kwa Kilatini: ukabidhi wa mamlaka) la kuwa mamlaka ya Kaisari yaliyokuwa na Waroma wa Kale na sasa yalikabidhiwa kwa Wajerumani.

Karolo aligawa urithi wake kati ya wanae na hii ilikuwa chanzo chaUfaransa upande wa magharibi na Ujerumani upande wa mashariki. Cheo cha Kaisari kiliendelea upande wa mashariki. Hivyo Ufaransa iliendelea kuwa ufalme wa nchi moja lakini upande wa mashariki Wajerumani waliunganishwa pamoja na watu jirani chini ya Kaisari aliyekuwa pia mkuu wa Italia ya Kaskazini,Bohemia (Ucheki) na sehemu mbalimbali ambazo leo hii ni ama Ufaransa au Ubelgiji na Uholanzi.

Mjerumani wa kwanza aliyepokea ukaisari kutoka kwaPapa waRoma alikuwaOtto I mwaka962.

Dola likaendelea hadi1806 wakatiNapoleon alipolifuta.

Jina la "Dola Takatifu la Kiroma" lilianza kutumiwa tangu1100 likaitwa baadaye pia "Dola Takatifu la Kiroma la Wajerumani".

Matatizo ya Dola

[hariri |hariri chanzo]

Hadikarne ya 13 dola lilikuwa na nguvu. Baadaye maeneo ndani yake yalijiongezea kiwango cha kujitawala. Kila Kaisari alichaguliwa na kamati ya makabaila na watemi wakuu. Kabla ya uchaguzi Makaisari walipaswa kuahidi ya kwamba wataheshimu haki ya makabaila juu ya maeneo yao. Mwishoni maeneo yalikuwa kamanchi huru kabisa yaliyoendelea kujitawala, kuendeshavita dhidi ya majirani kufuatasiasa zao.

Mwishoni dola lilikuwa za zaidi ya maeneo 300 ya kujitegemea; mengine makubwa kama Austria naPrussia, mengine madogo mno yenye eneo lamji mmoja tu.

Tangukarne ya 16 dola halikuwa na uwezo tena wa kufuata siasa ya nje kwa pamoja isipokuwa dhidi yaWaturukiWaosmani walioshambulia mara mbiliVienna,mji mkuu wa makaisari (1529 na1683).

Lakini vita vya kuwasukuma Waturuki watoke katika maeneo ya Ulaya ya kusini-mashariki waliyowahi kuvamia viliendeshwa na Kaisari kama mkuu wa Austria bila ya msaada wa dola takatifu.

Dola lilifaulu kwa kiasi fulani kutunzaamani au angalau kuepuka vita kati ya maeneo yake. IsipokuwaVita ya Miaka 30 kati ya1618 na1648 ilionyesha uwezo mdogo wa dola na karibu theluthi moja ya wakazi wa Ujerumani walikufa.

Tangukarne ya 17 majirani kama Ufaransa naSweden walijiingiza zaidi na zaidi katika siasa ya Ujerumani na maeneo makubwa kama Prussia hayakujali tena maazimio ya Kaisari. Dola Takatifu likaendelea kudhoofika.

Vita vya Napoleon vilimaliza mabaki yake.

Madola ya Kale
Karne za Kati
Madola ya karne 5 za mwisho
Madola ya kikoloni
Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuDola Takatifu la Kiroma kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Dola_Takatifu_la_Kiroma&oldid=1208186"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp