Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Delta ya Nile

Majiranukta:30°54′N31°7′E / 30.900°N 31.117°E /30.900; 31.117
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

30°54′N31°7′E / 30.900°N 31.117°E /30.900; 31.117

NASA picha ya satelite ya delta la MtoNile katika rangi za kubuni

Delta ya Nile (Kiarabu:دلتا النيل‎) nidelta yamtoNile iliyopo upande waKaskazini mwa nchi yaMisri ambapo ndipo mto Nile unapoanza kusambaa na hatimaye kuishia katikaBahari ya Mediteranea. Delta hii ni moja kati ya delta kubwa zaididuniani. Imeanzia upande waMagharibi ilipoAlexandria hadiPort Said kwa upande waMashariki.

Jiografia

[hariri |hariri chanzo]

Delta hii inachukua kiasi chakilometa 249 zaufukwe wa bahari ya Mediterania na pia katika eneo hili hufanyika shughuli mbalimbali zakilimo. Kuanzia upande wa Kaskazini hadiKusini delta hii inakadiriwa kuwa naurefu wa kilometa 160. Delta hii inaanzia taratibu chini kuanzia katikamji waCairo.

Mto Nile na Delta

Wakati mingine delta hii, hugawanywa katika vijisehemu vya Mashariki na Mashariki. Huku mto Nile wenyewe ukigawa mikono mito miwili yaaniDamietta naRosetta. Ikiwa inatiririkia katika bahari ya Mediteranea pia huwa na majina hayohayo.

Zamani, delta hii ilikuwa na mikono mito mbalimbali, lakini mikono mito hii ilipotea kutokana na jitihada za kuzuiamafuriko, kwa kukinga na kubadilisha mwelekeo. Moja kati ya mikono mito iliyopotea ni ule waWadi Tumilat.

Mfereji wa Suez (Suez Canal) unatiririka kuelekea Mashariki mwa delta na kuingia katikamwambao waZiwa Manzala kwa upande wa Kaskazini-Mashariki wa delta. Kwa upande wa Kaskazini-Magharibi pia kunamaziwa mengine matatu ambayo niZiwa Burullus,Ziwa Idku naZiwa Maryut.

Mto Nile kutoka juu unaonekana kamapembetatu. Pande za delta hii zinaonekana kumong’onyoka na baadhi ya mikono mito inaonekana kupanuka wakati ikiwa inaingia katika bahari ya Mediterania. Kutokana na kujengwa kwabwawa laLambo la Aswan kumepunguza kuja kwarutuba katika maeneo ya delta na hivyo kusababishawakulima kutumiambolea nyingi ili kurejesha hali ya rutuba katika maeneo ya kufanyia shughuli za kilimo katika eneo la delta. Sehemu yaudongo wa juu katika eneo la delta ni karibu na hatua 70 kwenda chini.

Historia

[hariri |hariri chanzo]
Matawi ya Delta la Mto Nile na maeneo ya jirani

Watu wamekuwa wakiishi katika eneo la delta ya mto Nile kwa miaka zaidi yaelfu kadhaa, na pia wamekuwa wakifanya shughuli za kilimo cha hali ya juu. Mto Nile umekuwa ulifurika katika kipindi chamwaka angalau mara moja, lakini hali hii imekuwa ikipungua kutokana na kutengenezwa kwa bwawa la Aswan.Kumbukumbu za siku za kale zinaonesha kuwa, Delta imekuwa na milango mito kadhaa.

Kwa upande wa Mashariki hadi magharibi, milango mito ni kama, Tanitic, Mendesian, t Phatnitic au Phatmetic[1]), pia kuna milango mito ya Sebennytic, Bolbitine, na Canopic pia hujulikana kama Herakleotic. Kwa sasa kuna milango mito miwili tu, hii ni kutokana na jitihada za kuzuia mafuriko na kuporomoka kwa pande za milango mito, milango mito hiyo ni pamoja na: Damietta uliopo kwa upande wa Mashariki, na Mlango mto wa Rosetta[2]. Mlango mto huu wa Damietta upo upande wa Magharibi wa delta.

Rosetta Stone lilipatikana katika delta ya mto Nile mwaka1787, katikabandari ya Rosetta. Katika enzi zaFarao, Delta hii ilikuwa ikijulikana kamaMisri ya Chini na pia ilikuwa ikiitwa "Goshen". Pia kuna sehemu kadhaa za kihistoria katika eneo la delta.[3]

Idadi ya Watu

[hariri |hariri chanzo]

Kiasi chanusu ya wakazi wa Misri, yaani kiasi chawatumilioni 80 huishi katika eneo la delta. Kwa upande wa nje kidogo ya mji mkubwa,wastani wamsongamano wa watu ni kiasi cha watu 1,000 kwa kilakilometa mraba mbili au zaidi. Mji waAlexandria ndio mji mkubwa kuliko yote katika eneo la delta na kukadiriwa kuwa na kiasi cha watu milioni 4. Miji mingine mikubwa katika eneo la delta ni pamoja naShubra al Khaymah,Port Said,El-Mahalla El-Kubra,El Mansura,Tanta, naZagazig.[4]

Wanyama na Mimea

[hariri |hariri chanzo]
Whiskered tern

Katika kipindi cha mwisho wa mwaka eneo la mto Nile huwa lina mwonekano mwekundu na kuwa namaua yalotus flowers. Upande wa chini wa eneo la Nile, yaani upande wa Kaskazini, na upande wa juu yaani upande wa Kusini, kunamimea mbalimbali inayoota kwa wingi. Mimea inayoota kwa wingi katika eneo la Mto Nile kwa upande wa chini ni yale yanayoitwa Egyptian lotus, na kwa upande wa juu hujawa na mimea inayoitwaCyperus papyrus au (papyrus sedge), japokuwa mimea hii haioti kwa wingi wakati huu kama ulivyokuwa hapo awali.

Zaidi ya aina elfu moja yandege, hupatikana katika eneo la delta, ikiwa ni pamoja na ndege aina yalittle gull nawhiskered tern. Pia ndege wengine wanaoishi katika eneo la delta ni pamoja nagrey heron,Kentish Plover,shovelers nacormorant. Pia hupatikana katika eneo hili la delta.

Wanyama wengine wanaopatikana katika eneo la delta ya Nile ni pamoja navyura,hua,kobe nanguchiro, lakini pia kunamamba naviboko: wanyama hawa wawili walikuwa wameenea sana katika eneo la delta katika siku za nyuma lakini siku hizi hali haipo hivyo. Aina zasamaki wanaopatikana katika eneo la delta ni pamoja na samaki wa aina yaStriped mullet.

Hali ya Hewa

[hariri |hariri chanzo]

Delta ya mto Nile inatabia za Kimediterania, ambayo huwa na sifa yamvua kidogo, kiais chamililita 100 hadi 200 kwa wastani wa mwaka na hata hivyo mvua hizi hunyesha wakati wa miezi yabaridi. Eneo la delta huwa na kipindi chajoto katika miezi yaJulai naAgosti kiasi chanyuzijoto 30 °C hadi nyuzijoto 48 °C. Kipindi cha baridi huwa ba kiasi cha nyuzijoto 10° hadi 19 °C. Eneo la delta huwa na hali yaunyevunyevu katika kipindi cha miezi ya baridi. Eneo la Delta limekuwa likimong’onyoka kwa wastani wa kilometa 502 kwa mwaka{{Fact|date = Aprili 2008 na inatabiriwa kuwa eneo la delta litakuwa limeisha hadi kufikia mwaka2550.

Ugatuzi

[hariri |hariri chanzo]

Miji ya kale na ya sasa eneo la Delta

[hariri |hariri chanzo]

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  1. Wilson, Ian.The Exodus Enigma (1985), page 46. London: Wiedenfeld & Nicolson.
  2. Hayes, W. 'Most Ancient Egypt', p. 87, JNES, 23 (1964), 73-114.
  3. Location of the siteIlihifadhiwa 15 Januari 2010 kwenyeWayback Machine., Kafr Hassan Dawood On-Line, with map of early sites of the delta.
  4. City Population website, citing Central Agency for Public Mobilisation and Statistics Egypt (web), accessed 11 Aprili 1908.

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Delta_ya_Nile&oldid=1151519"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp