Chuo Kikuu nitaasisi yaelimu ya ngazi ya juu ambako wanafunzi wanafundishwa na wataalamu wa fani mbalimbali ambao hufundisha pamoja na kuendeshauchunguzi wa elimu mpya.
Wanafunzi husoma kwenye chuo kikuu kwa shabaha ya kupata elimu hadi kupita mitihani yashahada au digrii kama vile yabachelor (ya kwanza), ya uzamili (master) (ya pili) na yauzamivu, PhD (ya tatu).
Siku hizi chuo kikuu kinatakiwa kuwa na sifa kadhaa za kukitofautisha na vyuo au taasisi nyingine kama vile:
kuunganisha fani mbalimbali kwa kukitofautisha na vyuo vinavyofundisha fani moja tu; kwa mfano chuo chaualimu, chuo chateolojia, chuo chauganga. Hata hivyo kuna vyuo vikuu vinavyokazia na kufundisha hasa upande mmoja wa elimu
kuunganisha kazi ya kufundisha na kazi ya uchunguzi kwa kukitofautisha na taasisi za uchunguzi zisizolenga mafundisho ya wanafunzi wa kawaida isipokuwa kuna nafasi ya kupata udokta
kutoa mafundisho ya ngazi ya juu inayokubaliwa kimataifa
kwa kawaida chuo kikuu kinatakiwa na kiwango kikubwa cha kujitawala nauhuru wa taaluma. Hali halisi hii inategemeamazingira: kuna tofauti kubwa kati nchi na nchi. Kufaulu katika maendeleo ya uchunguzi kunahitaji uhuru wa kuangalia, kuelewa na kujadili mawazo nafikra kutoka pande zote zadunia hata kama mawazo kadhaa hayakubaliwi katika mfumo wa kisiasa au kijamii ya nchi yenyewe.
Jamii katika tamaduni mbalimbali zilianzisha taasisi maalumu kwa elimu ya ngazi ya juu. Kati ya vyuo vya kwanza vinayofanana kiasi na chuo kikuu cha kisasa kuna hasa taasisi katikaUhindi,Ugiriki ya Kale,Uajemi,Ulaya na nchi za Kiislamu.
Mfumo wa kufundisha na kuratibu elimu ulio msingi wa vyuo vikuu vya kisasa ulianza hasa katika Ulaya yakarne za kati.
Vyuo hivi vya Ulaya viliendelea kuwa mahali pamaendeleo na kukuzasayansi ya kisasa. Kutoka hapa mfumo wa chuo kikuu pamoja na utaratibu wa ngazi zake za elimu ulisambaa kote duniani.
Kitovu cha kwanza cha elimu ya hali ya juu baraniAfrika kilikuwamaktaba ya Aleksandria nchiniMisri lakini ilikuwa taasisi ya kukusanya vitabu na mahali pa uchunguzi, si mafundisho.
Kihistoria vyuo vya kwanza vilivyotoa mafundisho kwenye hali ya juu ya kimataifa ya wakati wake vilikuwa chuo chaAl-Karaouine mjiniFes,Moroko tangu mwaka859 BK naAl Azhar mjiniKairo,Misri tangu mwaka975.