Ngamia waAsia yuko katika kanda inayoanziaAnatolia hadiManchuriakaskazini mwaChina. Amezoea zaidi baridi yaAsia ya Kati; wakati wa majira barafu halijoto ya mazingira inafikia -30°C. Joto kali inampa matatizo kidogo na kumchelewesha.
Umbile lao limelingana na mazingira ya jangwani.Miguu ni mipana na kuzuia wasizame chini kwenyemchanga.Nywele ni ndefu, hivyo zinakinga dhidi ya joto na baridi.
Nundu ni mahali pastoo ya akiba yamafuta; kama ngamia anapitia mahali pasipochakula anatumia mafuta kwanishati ya mwilini. Hahitaji kula kwa kipindi hadi siku 30.
Wanaweza kushikalita 100–150 mwilini na kuendelea jangwani bila kunywamaji kwawiki mbili. Penye majani mabichi ya kutosha, na kama joto si kali mno, ngamia anaweza kuendelea bila kunywa kwa wiki kadhaa.
Shingo ni ndefu kwa sababu kwa chakula anapendelea majani ya miti na vichaka.
Maisha
Ngamia wa Asia (C. bactrianus) ana nundu mbili
Ngamia ni wanyama wa kijamii na kwa asili huishi katika makundi yadume mmoja na majike kadhaa. Siku hizi kuna ngamia wa Asia mamia kadhaa kwenye pori ambao ni mabaki ya ngamia pori wa zamani. Wako China naMongolia.
Ngamia nundu-moja si wanyama wa pori asilia tena; inaaminiwa walitokea Uarabuni. Lakini kuna wanyama waliotoroka huko Australia na Amerika wanaoishi peke yao, hawafugwi.
Ngamia na binadamu
Binadamu akiongozana na ngamia
Ngamia wamefugwa nabinadamu tangu miaka 5,000–6,000 iliyopita. Leo hii mifugo hao ni takribanmilioni 19 na idadi kubwa, yaani milioni 14, wako Afrika, milioni 7 pekee nchini Somalia na milioni 3.3 nchiniSudan.
Watu hufuga ngamia kwa kubeba watu na mizigo. Nywele zao ni aina yasufu inayotumiwa kutengenezea mashuka, mahema na pia vitambaa vyanguo. Wanachinjwa kwanyama yao.
Ngamia hukamuliwa pia kamang'ombe. Katika nchi yabisi kiasi chamaziwa yao yanalingana na ya ng'ombe.
Katika miaka ya nyumaWamasai waKenya na piaTanzania wameanza kufuga ngamia baada ya kuona ya kwamba ng'ombe zao walikufa wakati wa ukame lakini ngamia waliendelea kuishi na kutoa maziwa.
Ngamia anachukua chakula chake kwenye mti wenye mizizi mirefu kushinda manyasi yanayoliwa na ng'ombe. Kwa sababu hiyo manyasi hukauka haraka wakati wa ukame kuliko majani ya miti.
Katika Biblia
Katika mazingira ambakoBiblia iliandikwa, ngamia alikuwa mnyama mkubwa kuliko wote wanchi kavu. Ndiyo sababu alitumika katikamethali mbalimbali kwa kusisitiza jambo.
Gilchrist, W. (1851).A Practical Treatise on the Treatment of the Diseases of the Elephant, Camel & Horned Cattle: with instructions for improving their efficiency; also, a description of the medicines used in the treatment of their diseases; and a general outline of their anatomy'. Calcutta: Military Orphan Press.