Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Brazil

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Shirikisho ya Brazil
República Federativa do Brasil
Kaulimbiu: Ordem e Progresso
"Order and Progress"
Wimbo wa taifa: Hino Nacional Brasileiro
"Brazilian National Anthem"
Mahali pa BrazilMahali pa Brazil
Mji mkuu
na mkubwa
Brasília
Lugha rasmi
Kabila
Dini
  Luiz Inácio Lula da Silva
Rais
  Geraldo Alckmin
Makamu wa Rais
Historia
  Kujitenga kutoka Ureno
7 Septemba 1822
  Kutambuliwa
29 Agosti 1825
  katiba
5 Oktoba 1988
Eneo
  Jumlakm2 8,515,767 km²(ya 5)
  Maji (asilimia)0.65%
Idadi ya watu
  Kadirio la 2024212,583,750
  Msongamano23.8/km²/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2024
  Jumla $4.891 trilioni
  Kwa kila mtu $22,928
PLT (Kawaida)Kadirio la 2024
  Jumla $2.307 trilioni
  Kwa kila mtu $10,816
HDI (2023) 0.786
juu
Gini (2022)52
SarafuReal (R$) (BRL)
Majira ya saaUTC−02:00 hadi −05:00 (BT)
Msimbo wa simu+55
Jina la kikoa.br

Brazil piaBrazili, rasmiJamhuri ya Shirikisho ya Brazil, ni nchi kubwa zaidi katikaAmerika ya Kusini naAmerika ya Kilatini. Ikiwa na kilomita za mraba milioni 8.5 na zaidi ya watu milioni 220, Brazili ni nchi ya tano kwa ukubwa duniani kwa eneo na ya saba kwa watu wengi zaidi.Mji mkuu wake niBrasília, na jiji lake lenye watu wengi zaidi niSão Paulo. Shirikisho ya Brazil hilo linaundwa na muungano wa majimbo 26 na Wilaya ya Shirikisho. Ndiyo nchi kubwa zaidi kuwa naKireno kama lugha rasmi na ndiyo pekee katika bara laAmerika. Pia ni moja ya mataifa yenye tamaduni nyingi na tofauti za kikabila, kutokana na zaidi ya karne ya uhamiaji mkubwa kutoka duniani kote. Pamoja na nchi yenye watu wengi zaidi yaWakatoliki wa Roma.

Ikipakana naBahari yaAtlantiki upande wa mashariki, Brazili ina ufuo wa kilomita 7,491. Inapakana na nchi na maeneo mengine yote ya Amerika ya Kusini isipokuwaEkuador naChile na inashughulikia 47.3% ya eneo la ardhi labara. Bondelake la Amazon linajumuishamsitu mkubwa wa kitropiki, makazi yawanyamapori wa aina mbalimbali, anuwai yamifumo ya ekolojia, na maliasili nyingi zinazozungukamakazi mengi yaliyolindwa. Urithi huu wa kipekee wa mazingira unaifanya Brazili kuwa mojawapo ya nchi 17 za megadiverse, na ni mada inayovutia sana kimataifa, kwaniuharibifu wa mazingira kupitia michakato kama vileukataji miti una athari za moja kwa moja kwa masuala ya kimataifa kama vilemabadiliko ya hali ya hewa na upotezaji wabioanuwai.

Brazili ni nguvu ya kikanda, na pia imeainishwa kama nchi yenye uchumi unaoibukia, ikiwa na nchi kubwa zaidi katika Amerika ya Kilatini. Kama uchumi wa kipato cha juu cha kati naBenki ya Dunia na nchi mpya iliyoendelea kiviwanda, Brazili ina sehemu kubwa zaidi ya utajiri wa kimataifa huko Amerika ya Kusini. Lakini nchi inashikilia viwango vinavyoonekana vyarushwa,uhalifu na ukosefu wausawa wa kijamii.

Jiografia

[hariri |hariri chanzo]

Misitu mipana yadunia inapatikana Brazil katika beseni yamto Amazonas. Misitu hii inafunika takriban 40% ya eneo la nchi.

Idadi kubwa ya wakazi hukalia maeneo karibu na pwani ya Atlantiki.

Kitovu chakilimo ni nyanda za "cerado" ausavana katika magharibi ya kati ya Brazil.

Mlima wa Corcovado nasanamu yaYesuMwokozi (Rio de Janeiro)

Mlima mkubwa niPico da Neblina (mita 3,014 juu yaUB) pamoja naPico 31 de Março (mita 2,992) ulio karibu nao kwenye mipaka ya Brazil, Venezuela na Guyana.

Mlima mkubwa wa kusini niPico da Bandeira (mita 2.891).

Mlima unaojulikana zaidi si mkubwa lakini uko ndani ya mji wa Rio de Janeiro: niCorcovado wenye mita 710. Juu yake kuna sanamu yaYesu Kristo ambayo niishara ya mji.

Mito muhimu

[hariri |hariri chanzo]
Ramani ya mwendo wa Amazonas inayovuka bara lote.

Brazil ina mto mkubwa na mrefu wa dunia ambayo niAmazonas wenye urefu wa takribankilometa 7000.Matawimto yake muhimu niRío Purús,Rio Negro naRio Tapajós.

Katika mashariki kuna mtoIguaçu wenyemaporomoko ya Iguaçu ambayo ndiyo makubwa duniani.

Maporomoko ya Iguaçu karibu nampaka wa Argentina/Brazil/Paraguay
Fortaleza

Parana (3.998 km) ni mto mrefu duniani baada ya Amazonas. Unalisha kituo kikubwa chanishati yamaji duniani chaItaipú.

Lagoa dos Patos karibu naPorto Alegre ni wangwa kubwa la Brazil lenye 10.000 km².

Ipiranga si mto mkubwa, hata kama jina lake linapatikana katikawimbo wa taifa.

Brazil inavisiwa vichache vidogo katika Atlantiki kama vileː

Visiwa hivyo ni sehemu yamgongo kati wa Atlantiki; hali halisi ni vilele vya milima inayoanza kwenye msingi wa bahari.

Kisiwa kikubwa cha Brazil hakipo baharini bali kati ya mto Amazonas: niMarajó, chenye eneo lakm² 48.000 (kubwa kushinda eneo laUswisi).

Hali ya hewa

[hariri |hariri chanzo]

Hali ya hewa ni ya kitropiki isipokuwakusini.

Beseni ya Amazonas inamvua nyingi. Kwenye milima ya kusiniusimbishaji unaweza kutokea kamatheluji.

Miji muhimu

[hariri |hariri chanzo]
São Paulo inazidi wakazi milioni 20
Rio de Janeiro
Curitiba, kusini mwa Brazil

Jiji kubwa niSão Paulo linalofikia (pamoja na mitaa ya jirani) kwenye idadi ya wakazi milioni 20.5.

Majiji ya kufuata niRio de Janeiro (wakazi milioni 11.4),Belo Horizonte (wakazi milioni 4.3),Curitiba (wakazi milioni 4),Recife (wakazi milioni 3.6),Brasilia (wakazi milioni 2.9),Salvador da Bahia (wakazi milioni 2.9),Fortaleza (wakazi milioni 2.6).

São Paulo ni jiji kubwa kabisa linalokua haraka sana. Ni moyo wa uchumi wa Brazil wenye viwanda vingi.

Rio de Janeiro ilikuwamji mkuu wa nchi hadi kuanzishwa kwa Brasilia. Imejulikana kote duniani kutokana nauzuri wamazingira yake nasherehe yaKanivali. Ina pia viwanda muhimu na ni kitovu chautamaduni wa nchi.

Mji mkuu waBrasilia ulijengwa kama ishara yaumoja wa nchi katika miaka mitatu tu.

Jumla yaasilimia 70 za wakazi hukalia miji mikubwa. (AngaliaOrodha ya miji ya Brazil.)

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Brazil imekaliwa na watu tangu miaka 10,000 iliyopita.Waindio waliingia kutoka kaskazini. Hakuna taarifa za kimaandishi lakiniakiolojia imeweza kufumbua makazi mbalimbali ya wenyeji asilia.

Brazil ilikuwa koloni laUreno hadi mwaka1822 kutokana namkataba wa Tordesillas ambamoHispania na Ureno zilipatana tarehe5 Septemba1494 kuhusu ugawaji wa dunia kati yao baada ya fumbuzi zaKolumbus.

Mreno wa kwanza aliyefika mwambao wa Brazil tarehe22 Aprili1500 alikuwaPedro Alvares Cabral. Makazi ya kwanza ya Wareno ni mji waSão Vicente mwaka1532. Mji mkuu wa kwanza ulikuwabandari yaSalvador da Bahia tangu1549.

Wareno walianzishakilimo chamiwa wakiwalazimisha Waindio kuwafanyia kazi. Walianza kuingia ndani ya bara wakitafutawatumwa kwa ajili ya mashamba nadhahabu.

Hali ya Waindio

[hariri |hariri chanzo]

Wenyeji walipungua haraka kwa sababu ya kuambukizwa magonjwa ya kigeni wakikosakinga dhidi yake, halafu kutokana na kutendewa vibaya kama watumwa mashambani.

Wareno walianza kutafutawafanyakazi penginepo kwa kuchukuawatumwa kutokaAfrika.

Mapadri Wajesuiti

[hariri |hariri chanzo]

Katika hali hiyowamisionariWakristo waShirika la Yesu walisimama upande wa Waindio. Walijipatia tamko rasmi laPapa waRoma la kuwa Waindio nibinadamu kamili, hivyo hawafai kutendewa kinyama. Wakibatizwa na kuwa Wakristo walitakiwa kukubaliwa kamaraia yeyote waUreno – amri ambayo mara nyingi haikukubaliwa na wavindaji wa watumwa na wenye mashamba.

Mapadri wa Shirika la Yesu walianzisha „reduciones“ yaani vijiji na miji kwa ajili ya Waindio walioishi chini yaulinzi wao na kutetewa dhidi ya wavindaji wa watumwa. Katika makazi hayo Waindio walifundishwashule kwalugha za kienyeji na Kireno, na kupata mafunzo waufundi mbalimbali. Kwa namna hiyo mapadri hao walitawala maeneo makubwa ndani ya bara.

Hali hiyo ilisababishahasira yawanasiasa Wareno walioendelea kuwapinga hadi Ureno penyewe. Hatimaye mwaka1767 hao mapadreWajesuiti walilazimishwa kuondoka katika Ureno na makoloni yake yote.

Upanuzi wa Brazil

[hariri |hariri chanzo]

Karne ya 17 naya 18 iliona kuanzishwa kwa miji mizuri kwa sababudhahabu naalmasi zilivumbuliwa katika misitu ya beseni ya Amazonas. Misafara ya kutafutahazina hizi zilipanua eneo la Brazil kuelekeamagharibi.

Mji mkuu ulihamishwa kwendaRio de Janeiro mwaka1763.

Uhuru 1822

[hariri |hariri chanzo]

Uhuru wa Brazil ulisababishwa nasiasa zaUlaya. Mwaka1807 Ureno ilivamiwa naUfaransa yaNapoleon Bonaparte. Mfalme wa UrenoJoão VI alikimbilia Brazil, Rio de Janeiro ikawa mji mkuu wa dola la Ureno.

Mfalme aliporudi Ureno mwaka1821 alimwachiamtoto wakePedro utawala wa Brazil. Mwaka1822 Pedro aliyeona mabadiliko ya kimapinduzi katika makoloni ya Hispania kote Amerika ya Kusini aliamua kutangazauhuru wa Brazil akiwa mwenyewe mfalme kwacheo chaKaisari.

Demografia

[hariri |hariri chanzo]

Asili/Kabila

[hariri |hariri chanzo]

Kwa mujibu wa sensa ya 2022 iliyofanywa naTaasisi yaJiografia naTakwimu ya Brazil (IBGE), Brazil ni moja ya nchi zenye mchanganyiko mkubwa wa kikabila duniani. Idadi ya watu inajumuisha asilimia 45.3 ya watu wamchanganyiko wa rangi (Pardo), asilimia 43.5%Weupe, asilimia 10.2Weusi, asilimia 0.6 Wenyeji wa asili, na asilimia 0.4 Waasia wa Mashariki, wengi wao wakiwa na asili yaKijapani. Watu wa mchanganyiko mara nyingi wana asili yaUlaya,Afrika, na Kiasili, hali inayoakisihistoria ya muda mrefu ya ukoloni na uhamiaji nchini humo.

Lugha rasmi na inayozungumzwa na watu wengi nchini Brazil niKireno, na hivyo kuifanya kuwa nchi kubwa zaidi inayotumiaKireno duniani. Kireno kinatumika katikaserikali,elimu, vyombo vya habari, na mawasiliano ya kila siku. Zaidi ya hapo, kuna zaidi ya lugha 200 za wenyeji wa asili zinazozungumzwa na jamii mbalimbali, japo nyingi ziko hatarini kutoweka. Katika baadhi ya maeneo, lugha za kikanda kama vileKijerumani na lahaja zaKiitaliano hutambuliwa rasmi kutokana na uwepo wa wakazi wa asili yaUlaya.

Brazil ni nchi yenye idadi kubwa yaWakristo, ambapo asilimia 75 ya raia wake walijitambulisha kamaWakristo mwaka 2022. Kati ya hao, asilimia 49 niWakatoliki wa Roma—urithi wa kipindi chaukoloni—na asilimia 26 ni Wakristo wa Kiinjili. Takriban asilimia 14 ya watuhawana dini, na asilimia 11 hawakutoa jibu kuhusu imani yao. Makundi madogo ya kidini ni pamoja na Wafuasi wa Uroho (Spiritism), dini za Kiafrika kamaCandomblé naUmbanda, pamoja naWaislamu,Wabuddha naWayahudi.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo yaAmerika Kusini

Argentina |Bolivia |Brazil |Chile |Ekuador |Guyana |Guyani ya Kifaransa |Kolombia |Paraguay |Peru |Surinam |Uruguay |Venezuela

Members
Observers
In Process
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Brazil&oldid=1449284"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp