Basi dogo huko Novoaltaisk.Basi la masafa marefu hukoKrakow,Polandi.
Basi (kutokaKiingereza "bus") ni chombo chausafiri kinachotumika kusafirishawatu kutoka eneo moja kwenda eneo jingine kwa ajili ya shughuli mbalimbali, kwa mfanokazi,masomo,utafiti na kadhalika.
Vyombo hivi vipo vya aina mbalimbali, kwa mfano kuna mabasi madogo yanayobebaabiria wachache na kusafiriumbali wa kawaida, pia kuna mabasi makubwa yenye kubebawatu wengi kuanziahamsini na kuendelea namabasi hayo husafiri umbali mrefu: yanaweza kusafiri kutokanchi moja kwenda nchi nyingine bila kumpumzishwa.
Katikadunia ya sasa mabasi yanatumika sana katika shughuli mbalimbali, kwa mfano shughuli za kiuchumi kwa kusafirishawafanyakazi nawafanyabiashara katikanchi mbalimbali.
Kwa msaada wa vyombo hivyowatu wanaweza kufika sehemu nyingi kwa wakati na kwenyekazi zao kwa wakati; hali hii imesaidia kwa kiasi kikubwa kukuzauchumi wa nchi nyingiduniani.
Makala hii kuhusu mambo yateknolojia bado nimbegu. Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.