Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Barua

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
José Olaya (17891823),shujaa wauhuru waPeru, alisafirisha barua kwa wapiganaji wa uhuru katikavita dhidi yaHispania.

Barua niujumbe wa kimaandishi unaotumwa kwamtu mwingine au watu wengine. Inawezekana kumwachia mtu ujumbe wa kimaandishi yaani barua mahali fulani lakini mara nyingi barua inatumwa kwa njia ya mtume au shirika linalofanya kazi hiikibiashara.

Kwa kawaida siku hizi barua inaandikwa kwenyekaratasi ama kwakalamu ama kwataipureta ama kwa kutumiakompyuta naprinta. Karatasi ya barua hukunjwa na kuwekwa ndani yabahasha yenyejina naanwani ya mpokeaji juu yake. Siku hizi idadi kubwa ya ujumbe inaandikwa kwa njia yabaruapepe.

Neno barua

[hariri |hariri chanzo]

Neno barua linatokana naKiarabu chaOmani ٻروۑbarwe[1].

Neno lingine, pia lenye asili ya Kiarabu, niwaraka[2], linatumiwa zaidi kwa ujumbe wa maandishi maalumu, si barua ya kawaida.

Barua katika historia

[hariri |hariri chanzo]
Barua kutoka Mesopotamia, iliandikwa kwa mwandiko wa kikabari, mnamo1300 KK.

Barua za kale kabisa zinazojulikana zimehifadhiwa kutokaMesopotamia ya Kale ambako watu waliandika juu yavigae vya mwandiko wa kikabari kwa kutumiamwandiko wa kikabari. Labda kulikuwa na barua za kale zaidi lakini hazikuhifadhiwa hadi leo.

Wamisri wa kale walituma barua zilizoandikwa juu yapapiri,Wagiriki naWaroma wa Kale waliandika ujumbe juu yabapa zaubao zilizofunikwa kwaganda lanta. Baadaye barua muhimu ziliandikwa juu ya vipande vyangozi nyembamba vilivyoandaliwa kwa kusudi hii.

Watu wa kwanza wa kutumia karatasi walikuwaWachina wa Kale, baadayeteknolojia ikasambaaduniani.

Katika dunia ya kale barua zilisafirishwa na watu waliotumwa moja kwa moja namwandishi mwenyewe.

Katikafalme kubwa, kama vileUajemi ya Kale,China ya Kale,Misri ya Kale auDola la Roma, kulikuwa na mfumo wa watarishi waserikali waliobeba barua rasmi kati yaofisi ya mfalme na sehemu mbalimbali za ufalme, lakini hii ilikuwa kwa ujumbe rasmi hasa. Watu wengine walihitaji kutumiahuduma za wasafiri kamawafayabiashara na misafara yao.

Mara nyingi kulikuwa na vituo vya pekee kila baada yakilomita kadhaa ambako watarishi walisubiri kufika kwa barua pamoja nafarasi waliotunzwa katika vituo hivyo. Kwa njia hii Waroma waliweza kusafirisha ujumbe takriban kilomita 80 kilasiku, yaani ilichukua takriban siku 60 kupeleka barua kutoka Roma hadi Misri kwa njianchi kavu (kilomita 3,200). Kamahali ya hewa iliruhusu,usafiri kwajahazi muda huo uliweza kufupishwa kiasi.

Katika miaka 400 iliyopita makampuni ya binafsi na za serikali zimepanua huduma za kusafirisha na kufikisha barua. Kama nitaasisi ya serikali kwa kawaida huitwaposta.

Kuhusugharama, kuna mbinu mbiliː ama mpokeaji analipa gharama za usafirishaji wakati wa kupokea barua, au mwenye kutuma barua analipa gharama wakati wa kutuma. Nchi nyingi huwa na mfumo ambako mwenye kutuma ananunuastempu kwa gharama ya usafirishaji; stempu hizo ni vipande vya karatasi vyenyethamani maalumu ambavyo vinabandikwa kwagundi kwenye bahasha na kugongwamhuri ili zisitumiwe tena.

Umbo la barua

[hariri |hariri chanzo]

Katikahistoria ndefu ya matumizi ya barua ilitokea kawaida namna ya kutunga na kuandika barua. Bahasha au sehemu ya nje ya barua huwa na majina ya mpokeaji na pia ya mwandishi pamoja na anwani zao. Barua yenyewe huwa nahabari kuhusutarehe namahali pa kuandikwa, jina ausahihi la mwandishi, jina la mwandikiwa.

Barua zinatofautiana kama ni barua za binafsi ndani yafamilia, kati yamarafiki auwapenzi, kati ya wafanyabiashara auwateja na wauzaji, kati ya ofisi naraia na kadhalika.

Muundo wa barua ya kirafiki umegawanyika katika sehemu sita ambazo ni: Anwani ya mwandishi, Tarehe, Mwanzo wa barua, Kiini cha barua, Mwisho wa barua na Jina la mwandishi.

Barua na jamii

[hariri |hariri chanzo]

Barua ni chombo muhimu katikautamaduni wa kila jamii. Zinategemea kuwepo kwa watu wanaojua kusoma na kuandika. Si lazima ya kwamba kila mtu anayetuma barua au kuipokea anajua kuandika au kusoma, maana inawezekana kutumia msaada wa watu wengine. Lakinimawasiliano kwa barua ni uhamasisho mkubwa kwa watu kujifunza na kuboreshaelimu hiyo.

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  1. Tazama Sacleux, Dictionnaire Français—Swahili, "barua", anayerejea neno kwa lahaja ya Kiarabu cha Omani
  2. kutokakar. ورق "karatasi"
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Barua&oldid=1348090"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp