Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Bangladesh

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
গণপ্রজাতন্ত্রী বাংলােদশ
Gônoprojatontri Bangladesh

Jamhuri ya Watu wa Bangladesh
Bendera ya BangladeshNembo ya Bangladesh
BenderaNembo
Kaulimbiu ya taifa:
Wimbo wa taifa:Amar Shonar Bangla
"Bengali yangu ya dhahabu"
Lokeshen ya Bangladesh
Mji mkuuDhaka
23°42 N 90°22 E
Mji mkubwa nchiniDhaka
Lugha rasmiKibengali (Bangla)
SerikaliJamhuri
Abdul Hamid
Hasina Wazed
Uhuru
Ilitangazwa
Siku ya Ushindi
26 Machi1971
16 Desemba1971
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
147,570 km² (ya 94)
6.4
Idadi ya watu
 -2013 kadirio
 -2001 sensa
 - Msongamano wa watu
 
156,594,962 (ya 8)
129,247,233
1,033.5[1]/km² (ya 12)
FedhaTaka (BDT)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
BDT (UTC+6)
not observed (UTC+6)
Intaneti TLD.bd
Kodi ya simu+880 -SubCodes

-


Bangladesh (pia:Bangladesh; kwaKibengali: বাংলাদেশ, bāṃlādeś) ni nchi yaAsia ya Kusini. Imepakana naUhindi pande zote barani isipokuwa mpaka mfupi wakm 193 naMyanmar upande wa kusini-mashariki napwani yaGhuba ya Bengali.Ni nchi ya nane kwa kuwa na watu wengi zaidi duniani na miongoni mwa nchi zenye msongamano mkubwa wa watu na wakazi wanaozidi milioni 170 ndani ya eneo la kilomita za mraba 148,460.Dhaka ndio mji mkuu na jiji kubwa zaidi, ni kituo cha kitaifa cha kisiasa, kifedha na kitamaduni

Jiografia

[hariri |hariri chanzo]

Sehemu kubwa ya nchi nidelta yamitoGanga naBrahmaputra.

Uso wa nchi nitambarare namita chache tu juu yauwiano wa bahari. Hivyo wananchi huteswa mara nyingi namafuriko makali.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Bangladesh ni sehemu yamashariki yaBengali ya kihistoria ambayo ilikuwa ndani yaUhindi wa Kiingereza hadi1947.

Mwaka1857 Wahindi walipingautawala waKampuni ya Kiingereza kwa Uhindi wa Mashariki. Matokeo yake utawala ulishikwa naserikali yenyewe yaUingereza kamakoloni (1858).

Mwisho wakarne ya 19harakati za Wahindi kutafutauhuru zilianza upya. Mwaka1885chama cha INC (Indian National Congress) kiliundwa naWahindu naWaislamu pamoja waliodai uhuru.

Mwaka1906 viongozi Waislamu walitoka katika INC na kuunda "Shirikisho la Waislamu".

Mwaka1917 Uingereza ulitamka ya kwamba ulitaka kuelekea polepole hali ya kujitawala kwa Wahindi. Viongozi wa wenyeji hawakuridhika na mkasi wa mabadiliko. Chini yauongozi waMahatma Ghandi mwendo wa kupigania uhuru bila mabavu ulipata nguvu. Ghandi alipigania hasaumoja wa Wahindu na Waislamu lakini alipingwa na viongozi wenyeitikadi kali wa pande zote mbili.

Baada yaVita Kuu ya Pili ya Dunia Waingereza walikubali kujiondoa katika Uhindi. Swali kubwa lilikuwa kama nchi itabaki kama nchi moja au kama maeneo ya Waislamu yatajitenga.

Tarehe 14/15 Agosti1947 utawala wa Uingereza ulikwisha. Bara Hindi iligawanywa katika nchi mbili zaUhindi na Pakistan.Mgawanyo wa Uhindi ulikuja navita na kumwaga kwadamu nyingi. Bengali yenyewe iligawanyika kwa sababu wakazi wengi wa mashariki walikuwaWaislamu, tofauti na Wabengali wengine waliokuwaWahindu.

Tarehe30 Januari1948 Ghandi mwenyewe aliuawa na Hindu mkali aliyemchukia kwa sababu alitakausawa wa Waislamu na Wahindu.

Wakati ule Bengali ya mashariki ilikuwa nchi moja pamoja naPakistan ya leo, bila kujali umbali mkubwa kati ya pande hizo mbili zilizounganishwa nadini.

Iliitwa "Pakistan ya Mashariki" mpaka mwaka1971 ilipojitenga na Pakistan kwa msaada wa India katikaVita vya Uhuru vya Bangladesh.

Watu

[hariri |hariri chanzo]

Kati ya nchi kubwa, Bangladesh inaongoza kwamsongamano wa watu.Uzazi umepunguzwa sana na kampeni zaudhibiti wake zilizofanywa miaka ya mwisho.

Wabengali niasilimia 98 za wakazi, lakini kuna piamakabila madogo 11.

Asilimia hizohizo wanaongeaKibengali, ambacho ndicholugha rasmi.Kiingereza pia kinatumika sana.

Upande wadini, Waislamu ni asilimia 86-90 (wengi wakiwaWasuni), Wahindu ni asilimia 8-12,Wabuddha ni asilimia 0.6 naWakristo (hasaWakatoliki, halafuWaprotestanti) asilimia 0.4.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Tanbihi

[hariri |hariri chanzo]
  1. World Bank Development Indicators Database, 2006.

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  • Baxter, C (1997).Bangladesh, from a Nation to a State. Westview Press.ISBN 0-8133-3632-5.OCLC 47885632.
  • Iftekhar Iqbal (2010) The Bengal Delta: Ecology, State and Social Change, 1840–1943, Cambridge Imperial and Post-Colonial Studies, Palgrave Macmillan, Pages: 288,ISBN 0230231837
  • M. Mufakharul Islam (edited) (2004) Socio-Economic History of Bangladesh: essays in memory of Professor Shafiqur Rahman, 1st Edition, Asiatic Society of Bangladesh,Kigezo:Oclc
  • M. Mufakharul Islam (2007), Bengal Agriculture 1920–1946: A Quantitative Study, Cambridge South Asian Studies, Cambridge University Press, Pages: 300,ISBN 0521049857
  • Meghna Guhathakurta & Willem van Schendel (Edited) (2013) The Bangladesh Reader: History, Culture, Politics (The World Readers), Duke University Press Books, Pages: 568,ISBN 0822353040
  • Sirajul Islam (edited) (1997) History of Bangladesh 1704–1971(Three Volumes: Vol 1: Political History, Vol 2: Economic History Vol 3: Social and Cultural History), 2nd Edition (Revised New Edition), The Asiatic Society of Bangladesh, Pages: 1846,ISBN 9845123376
  • Sirajul Islam (Chief Editor) (2003) Banglapedia: A National Encyclopedia of Bangladesh.(10 Vols. Set), (written by 1300 scholars & 22 editors) The Asiatic Society of Bangladesh, Pages: 4840,ISBN 9843205855
  • Srinath Raghavan (2013) ‘1971: A Global History of the Creation of Bangladesh’, Harvard University Press, Pages: 368,ISBN 0674728645

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Nchi na maeneo yaAsia

Afghanistan |Armenia2 |Azerbaijan |Bahrain |Bangladesh |Bhutan |Brunei |China |Falme za Kiarabu |Georgia2 |Hong Kong3 |Indonesia |Iran |Iraq |Israel |Jamhuri ya China (Taiwan) |Japani |Kamboja |Kazakhstan |Kirgizia |Korea Kaskazini |Korea Kusini |Kupro2 |Kuwait |Laos |Lebanoni |Macau3 |Malaysia |Maldivi |Mongolia |Myanmar |Nepal |Omani |Pakistan |Palestina |Qatar |Saudia |Singapuri |Sri Lanka |Syria |Tajikistan |Timor ya Mashariki |Turkmenistan |Ufilipino |Uhindi |Urusi1 |Uthai |Uturuki1 |Uzbekistan |Vietnam |Yemen |Yordani

1. Nchi ina maeneo katikaAsia naUlaya. 2. Nchi ikoAsia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi zaUlaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.
Makala hii kuhusu maeneo yaAsia bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuBangladesh kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Bangladesh&oldid=1429310"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp