Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Australia na Pasifiki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Australia na Visiwa vya Pasifiki
* AS:Samoa ya Marekani * AU:Australia * CK:Visiwa vya Cook * FJ:Fiji * FM:Mikronesia * GU:Guam (USA) * KI:Kiribati * MH:Visiwa vya Marshall * MP:Visiwa vya Mariana * NC:Kaledonia Mpya (Ufaransa) * NR:Nauru * NU:Niue (New Zealand) * NZ:New Zealand * PF:Polynesia ya Kifaransa * PG:Papua Guinea Mpya * PN:Pitcairn (Uingereza) * PW:Palau * SB:Visiwa vya Solomon * TL:Timor ya Mashariki * TK:Tokelau * TO:Tonga * TV:Tuvalu * US:Hawaii * VU:Vanuatu * WF:Wallis na Futuna (Ufaransa) * WS:Samoa ya MagharibiNchi za Asia * [BN]:Brunei * [CN]:China * [ID]:Indonesia * [MY]:Malaysia * [PH]:Ufilipino * [TW]:Taiwan

Australia na Visiwa vya Pasifiki (pia:Oceania, Okeania, Oshania) hujumlishwa mara nyingi pamoja katika hesabu ya mabara.

Hasa watu kwenyevisiwa vingi vyaPasifiki wanautamaduni wa karibu. Vilevilehistoria ya visiwa hivyo kabla ya kuenea kwaukoloni imefanana katika mengi.

Bara au la?

[hariri |hariri chanzo]

Hivyo mara nyingi sehemu hii yadunia imeitwa "Bara la Kiutamaduni".Jina hili si sahihikijiografia kwa sababu maeneo yake yako juu yamabamba ya gandunia tofauti, kama vilebamba la Pasifiki,bamba la Australia na mengine madogo. Hatawataalamu hawapatani kuhusu mipaka ya eneo hilo.

Jina

[hariri |hariri chanzo]

Kwalugha nyingi za dunia jina la "Oceania" (Okeania, Oshania) limekuwa la kawaida kutokana naneno laKigiriki "okeanos" (kwaKilatini: oceanus; kwaKiingereza: ocean). Hivyo "Oceania" yamaanisha "nchi katika bahari". Ila tu hatuoni faida ya kuingiza neno hili katika lugha yaKiswahili kwa sababu ni neno lisiloeleweka vizuri. Mara wataalamu hujadili "Oceania" kuwa visiwa vya Pasifiki pamoja naAustralia; mara wanaona "Oceania" ni visiwa vile pekee bila Australia na wengine wanasema wenyewe "visiwa vya Pasifiki" ingekuwa jina zuri zaidi kama Australia haihesabiwi.

"Australasia" imekuwa jaribio tofauti la kutaja eneo, hasa kati ya wataalamu wa Australia, ila tu halipendwi na watu wengi visiwani. Hivyo imetumiwa zaidi kwa kanda la Australia na visiwa jirani pekee.

Eneo

[hariri |hariri chanzo]

Visiwa vyote kwa pamoja (bila Australia yenyewe) hukadiriwa kuwa 7,500 vyenye eneo la nchi kavu lakilomita za mrabamilioni 1.3 vilivyosambaa katika eneo la bahari lakilomita za mraba milioni 70. Takriban visiwa 2,100 vimekaliwa nawatu milioni 14.9.

Jiolojia

[hariri |hariri chanzo]

Eneo hili si bara kwa maana yajiolojia. Visiwa vikubwa vyaNew Zealand,Guinea Mpya,Kaledonia Mpya naTasmania ni mabaki yabamba laGondwana ya kihistoria. Guinea Mpya imetenganishwa na Australia kwabahari ya Arafura isiyo nakina kirefu na wakati waenzi ya barafu iliyopita zilikuwa kama nchi moja kwa sababuuwiano wa bahari ulikuwa chini kuliko leo.

Visiwa vingi katika Pasifiki nimilima yavolkeno inayoinuka kutokatako la bahari hadi uso wamaji; mara nyingi zinaonyeshakasoko. Visiwa vingine vinajengwa namatumbawe yanayokua juu ya volkeno ambazo zimeishia kidogo chini ya uso wa bahari. Visiwa vingine niatoli ambako matumbawe yamejenga tuta tumbawe kwaumbo lamviringo kuzunguka kisiwa cha kivolkeno.

Sababu ya kutokea kwa volkeno nyingi ni miendo yagandunia katika tabaka zaganda la dunia chini ya bahari.Ngozi ya nje au ganda la dunia hufanywa na vipande mbamlimbali (=mabamba ya gandunia) vinavyoelea juu ya tabaka yamwambamoto nakiowevu. Pale ambako vipande hivi vinagusana mara kwajoto na mwamba moto ulioyeyuka unapanda juu; pale ambao kupanda huku kunatokea haraka tunaona volkeno na hivyo kisiwa kipya kutokea. Mfano ni safu ya visiwa vyaHawaii ambavyo nisafu ya milima ya volkeno inayoanza kwenye tako la bahari, mengine inaonekana kama visiwa, mengine iko chini ya uso wa bahari.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

AngaliaHistoria ya maeneo ya Pasifiki naHistoria ya Australia

Kanda

[hariri |hariri chanzo]

Mara nyingi kanda nne zimetofautishwa:

Maeneo yanayotajwa kwa "Melanesia" na "Australasia" huingiliana.

Nchi na Maeneo ya Australia na Visiwa vya Pasifiki

[hariri |hariri chanzo]

(Nchi huru zaonekana kwa mwandiko mzito, maeneo yaliyo chini ya nchi nyingine kwa mwandiko wa kawaida)

Jina la eneo,
pamoja nabendera[1]
Eneo
(km²)
Wakazi
(kadiro mnamo
1 Julai2002)
Msongamano
(watu kwenye km²)
Mji mkuu
Australasia (Australia naNew Zealand)
Australia
7,686,85020,697,2412.5Canberra
Kisiwa cha Krismasi (Australia)[2]
1354743.5The Settlement
Visiwa vya Cocos (Keeling) (Australia)[2]
1463245.1West Island
New Zealand[3]
268,6803,908,03714.5Wellington
Kisiwa cha Norfolk (Australia)
351,86653.3Kingston
Melanesia[4]
Fiji
18,270856,34646.9Suva
Sehemu zaIndonesia[5]
499,8524,211,5328.4Jakarta
Kaledonia Mpya (Ufaransa)
19,060207,85810.9Nouméa
Papua Guinea Mpya[6]
462,8405,172,03311.2Port Moresby
Visiwa vya Solomon
28,450494,78617.4Honiara
Vanuatu
12,200196,17816.1Port Vila
Mikronesia
Shirikisho la Mikronesia
702135,869193.5Palikir
Kiribati
81196,335118.8Teinainano
Visiwa vya Marshall
18173,630406.8Majuro
Nauru
2112,329587.1Yaren
Visiwa vya Mariana ya KaskaziniMarekani
47777,311162.1Saipan
Guam (Marekani)
549160,796292.9Hagåtña
Palau
45819,40942.4Melekeok[7]
Polynesia[8]
Samoa ya Marekani (Marekani)
19968,688345.2Fagatogo,Utulei[9]
Visiwa vya Cook (New Zealand)
24020,81186.7Avarua
Polynesia ya Kifaransa (Ufaransa)
4,167257,84761.9Papeete
Hawaii (Marekani)
29,3111,211,53742.75Honolulu
Niue (New Zealand)
2602,1348.2Alofi
Kisiwa cha Pasaka (Chile)
163,63,79123,17Hanga Roa
Visiwa vya Pitcairn (Uingereza)
54710Adamstown
Samoa
2,944178,63160.7Apia
Tokelau (New Zealand)
101,431143.1[10]
Tonga
748106,137141.9Nuku'alofa
Tuvalu
2611,146428.7Vaiaku
Wallis na Futuna (Ufaransa)
27415,58556.9Mata-Utu
Total9,008,45835,834,6704.0

Tanbihi

[hariri |hariri chanzo]
  1. Maeneo hutajwa kufuatana na mpangilio wa Umoja wa Mataifa. Maeneo kadhaa huhesabiwa ama kama nchi za kimabara au sehemu zaAsia auAmerika Kaskazini.
  2. 12Kisiwa cha Krismasi naVisiwa vya Cocos (Keeling) ni maeneo ya Australia katikaBahari Hindi kusini yaIndonesia hivyo hutazamia kuwa sehemu zaAsia ya Kusini-Magharibi.
  3. New Zealand mara nyingi huhesabiwa ndani yaPolynesia kulikoAustralasia.
  4. BilaTimor ya Mashariki na sehemu zaIndonesia ambazo ni visiwa vya Asia lakini huhesabiwa mara nyingi kati ya visiwa vya Pasifiki.
  5. <--Indonesia kwa jumla ni sehemu yaAsia ya Kusini-Mashariki; sehemu zaGuinea Mpya (Irian Jaya) naVisiwa vya Maluku .huhesabiwa humo
  6. [[Papua Guinea Mpya huhesabiwa upande wa Australia lakini pia kwaMelanesia.
  7. Tar7 Oktoba2006 serikali ilihamia Melekeok iliyoko takriban kilomita 20 kaskazini ya Koror.
  8. BilaHawaii ambalo ni jimbo la Marekani. Inahesabiwa mara nyingi kati ya eneo la Amerika ya Kaskazini ingawa ni funguvisiwa ndani ya Pasifiki.
  9. Fagatogo ni makao ya unge na mahakama yaSamoa ya Marekani;Utulei ni makao ya serikali.
  10. Tokelau ni eneo la New Zealand na haina makao makuu kwa jumla kila kisiwa kina chake.
Makala hii kuhusu eneo fulani bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.

Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Australia_na_Pasifiki&oldid=1154426"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp