Alikuwa kijana wa miaka 19 aliyejiandaa kuwaafisa wajeshi kwa mara ya kwanza katikamaisha yake aliposikia habari za kuuawa kwa Julius Caesar. Alikimbilia Roma mara moja alipopata habari ya kuwa Caesar alimsiliki na kumtaja kama mrithi katika wasia. Hapo aliamua kulipiza kisasi juu ya wauaji wa Caesar, hivyo akaingia katikasiasa ya Roma na kipindi cha vita vya wenyewe kwa wenyewe kilichofuata mauaji yakiongozi wa dola.
Rafiki yakemarehemu,Marcus Antonius, hakukubali wasia akatwaamali yote, lakini watu wengi nawanajeshi wa Caesar walisimama upande wa Octavius. Huyo aliajiriaskari na kujengajeshi na mwaka43 KK alitwaamji wa Roma kwa nguvu ya kijeshi wakati Marcus Antonius alikuwa mbali hukoGallia.
Senati ya Roma ilikubali hatua hii na kumchagua kuwaseneta. Aliendelea kuongoza jeshi la Senati na kumshinda Marcus Antonius kwenye mapigano hukoItalia ya Kaskazini.
Baada yaushindi huo alikubaliwa kamakonsuli wa Roma akaendelea kupatana na Marcus Antonius na kujengaushirikiano naye. Pamoja walitawala Roma baada ya kupewa na senatimadaraka ya kidikteta kwa muda wa miaka 5 na baadaye miaka 5 tena.
Mwaka42 KK walifaulu kuwashinda wauaji wa Caesar waliokaaUgiriki na baadaye waligawana eneo ladola kati yao: Octavianus alikuwa mkuu wa sehemu yamagharibi na Marcus Antonius mkuu wa sehemu zamashariki alipomwoaKleopatramalkia waMisri.
Mapigano ya baharini ya Aktium' ya 31 KK' (taswira ya 1672).Dola la Roma baada ya Augusto. kijani nyeusi: Majimbo chini ya Roma kijani nyeupe: maeneo lindwa chini ya Roma yenye kiwango cha kujitawala; kijani nyeupe nje ya mstari mweusi: Jimbo la Germania Magna lililopotea baada ya mwaka 9
Maelewano kati yao yalizorota na mwaka33 KK walitengana. Octavianus alimshinda Marcus katika mapigano yabaharini hukoAktium tarehe2 Septemba31 KK na huyo alijiua pamoja naKleopatra.
Baada ya kuvamia na kutekaMisri Octavianus alirudi Roma mjini mwaka29 KK akawa mtawala pekee.
Huko Roma alishangaza watu wote akirudishamamlaka yake ya kidikteta kwa senati. Aliombwa kuendelea kamamkuu wa jeshi akakubali.
Alikataa kupokea madaraka ya dikteta kwa muda wa maisha yake. Kwa njia hiyo alirudishakatiba yajamhuri iliyotawaliwa na senati na maafisa yake.
Lakini hali halisi alishika mamlaka yote kama mtawala mkuu aliyeheshimutaasisi za jamhuri. Nihekima hii iliyosifiwa na wengi ya kuwa hakuendelea kujipatia cheo chamfalme au cha dikteta akaridhika kuitwaraia wa kwanza.
Utawala wake ulileta kipindi kirefu cha amani ya ndani. Wananchi walioteseka kwa miaka ya vita vya wenyewe kwa wenyewe waliweza kujenga maisha upya nauchumi ulistawi.
Milki kubwa ya Misri ilikuwa sehemu ya Dola la Roma. Hata sehemu nyingi zaGermania ziliingizwa katika dola.
Vita vya pekee vilivyoenda vibaya vilikuwa jaribio la kupanua mipaka ya Roma katikaGermania hadimto Elbe. Wagermania waliangamizalegionitatu nampaka wa Kiroma ulirudishwa hadimto Rhine.
Makala hii kuhusuKaizari fulani waRoma bado nimbegu. Je, unajua kitu kuhusuAugusto kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.