Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Angola

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Angola
República de Angola (Kireno)
Kaulimbiu: "Virtus Unita Fortior" (Uadilifu ukiwa pamoja ni wenye nguvu zaidi)
Wimbo wa taifa: "Angola Avante" (Endelea Angola)
Mahali pa AngolaMahali pa Angola
Ramani ya AngolaRamani ya Angola
Mji mkuu
na mkubwa
Luanda
Lugha rasmiKireno
Lugha za taifaKichokwe
Kimbundu
Kikongo
Kiwambo
Kiluchazi
Kiumbundu
Kabila
SerikaliJamhuri ya urais wa kitaifa
 Rais
João Lourenço
Esperança da Costa
Uhuru kutokaUreno
  Uhuru
11 Novemba 1975
Eneo
  Jumlakm2 1,246,700
  Maji (asilimia)ndogo sana
Idadi ya watu
  Kadirio la 2025 39,040,039
  Msongamano31/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2023
  Jumla $260.323 bilioni
  Kwa kila mtu $7,077
PLT (Kawaida)Kadirio la 2023
  Jumladecrease $93.796 bilioni
  Kwa kila mtudecrease $2,432
HDI (2023) 0.616
Gini (2018)51.3
SarafuKwanza ya Angola (AOA)
Majira ya saaUTC+1 (WAT)
Msimbo wa simu+244
Jina la kikoa.ao

Angola (jina rasmi:Jamhuri ya Angola; kwaKireno:República de Angola) ni nchi yakusini mwa Afrika inayopakana naNamibia upande wa kusini,Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo upande wa kaskazini,Zambia upande wa mashariki, naBahari ya Atlantiki upande wa magharibi. Inajumuisha piamkoa wa Cabinda, uliotenganishwa na eneo kuu ulioko kaskazini mwaDRC.Mji mkuu niLuanda ambao pia ndio mji mkubwa nchini, ukifuatwa naHuambo naLobito. Angola ina wakazi takriban milioni 35, wakiifanya kuwa ya 42 duniani kwa idadi ya watu.Lugha rasmi niKireno hukuKiumbundu,Kimbundu naKikongo zikiwa lugha zinazozungumzwa zaidi nchini.

Angola ni nchitajiri kwamafuta namadini:almasi ndiyo muhimu zaidi. Lakini nchi nimaskini kutokana navita vya miaka 29; kwanza vita vya kupiganiauhuru dhidi yaUreno iliyofuatwa navita ya wenyewe kwa wenyewe hadi mwaka2002.

Jiografia

Maeneo ya Angola

Ramani ya Angola na Mikoa iliohesabiwa
Ramani ya Angola na Mikoa iliohesabiwa

Angola imegawiwa katika mikoa 18 (províncias),wilaya 162 (municípios) nakata 559.
Mikoa ni:

Historia

Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwawawindaji wa jamii yaWasani.

Katikakarne za kwanzaBK kutokakaskazini walifikawahamiajiWabantu wenyeujuzi wakilimo nauhunzi.

Kuanziakarne ya 14, falme mbalimbali zilienea sehemu za Angola, kwa mfanoDola la Kongo,Dola la Lunda naDola la Kasanje.

Asili na historia ya jina 'Angola'

JinaAngola linatokana naneno lalugha yaKibantu "N’gola", ambalo lilikuwa jina lakiongozi waufalme wa Ndongo na Matambakarne ya 16, ambapoWareno walianzaukoloni katika eneo hili.

Dola la Kongo

Ramani ya kihistoria ya Kongo

Dola la Kongo lilikuwaufalme ulioenea ndani ya nchi za leo zaAngola,Kongo (Kinshasa) naKongo (Brazzaville).

Ulianzishwa katikakarne ya 14 ikadumu hadikarne ya 17.

Mtawala wake alikuwa na cheo cha "Mwene Kongo" au "Manikongo" wakabila laBakongo.

Ufalme huo umejulikana zaidi kihistoria kwa sababu yamawasiliano yake ya kimataifa. Katikakarne ya 15meli zaWareno zilifikamwambaoni mwake.

Wakati wa kukutana na Wareno Ufalme wa Kongo labda ulikuwa na eneo lakm² 300,000 ukaunganisha robo ya magharibi ya Kongo (Kinshasa) pamoja na sehemu za Angola na Kongo (Brazzaville).

Manikongo mbalimbali walijenga uhusiano naUreno na Kongo ilikuwataifa la kushikamana na Ureno hadi kuharibika kwa uhusiano huo. Katika kipindi kiletaarifa mbalimbali ziliandikwa zinazotupa leo picha nzuri ya ufalme huo.

Manikongo alikaa katikamji waM'banza-Kongo.

Baada ya wafalme kuwaWakristoWakatoliki na kujengwa kwakanisa kuu, jina la "São Salvador do Congo" (kwaKireno: "Mwokozi Mtakatifu wa Kongo") lilikuwa kawaida kwa mji mkuu wamilki.

Ufalme ukawa na majimbo,wilaya navijiji. Majimbo yalikuwa saba yaMpemba,Nsundi,Mpangu,Mbata,Mbamba naSoyo.

Kwa mikataba ya baadaye falme zaKakongo,Loango naNgoy likatokeashirikisho ya sehemu nne.

Dola la Lunda

Dola la Lunda lilikuwaufalme waKibantu katika miaka1600 hadi1850 hivi kandoni kwamto Kasai, mpakani kwa nchi za kisasa zaAngola naJamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Dola la Kasanje

Dola la Kasanje lilikuwaufalme waKibantu katika miaka1620 hadi1910 hivi kandoni kwamto Kwango, upande wakaskazini wa nchi ya kisasa yaAngola. Lilianzishwa na viongozi kutokaDola la Lunda.

Mwaka 1910 lilivamiwa naWareno na kuingizwa katikakoloni lao la Angola.

Dola la Ndongo

Eneo laUfalme wa Ndongo.

Dola lingine la kusini lilikuwa lile la Ndongo, lililopambana na Wareno miaka 30 chini yamalkiaNjinga katikakarne ya 17.

Vita vya uhuru

Mwaka1966Jonas Savimbi alianzisha tapo laUNITA (kwaKireno:União Nacional para a Independência Total de Angola) kama harakati ya kukomboa Angola kutokaukoloni waUreno. UNITA ilikuwa moja kati ya harakati tatu zilizoshindana.

UNITA ilianza kama kikundi chakikomunisti kufuatana naitikadi yaMao Zedong. Uadui kati ya Wakomunisti waUchina naUrusi ulionekana katika mashindano ya UNITA dhidi yaMPLA (kwa Kireno: Movimento Popular de Libertação de Angola - Partido do Trabalho) iliyosaidiwa na Urusi.

Vita vya wenyewe kwa wenyewe

Baada yauhuru mwaka1975 MPLA ilitawalamji mkuu na kuundaserikali rasmi lakini Savimbi aliendelea kuipinga.

Savimbi alipata kupokea baadaye usaidizi kutoka maadui wote wa MPLA bila kujali itikadi. UNITA ilipata misaada toka serikali mbalimbaliduniani ili kuiondoamadarakani serikali ya MPLA. Savimbi alikuwa akipata misaada yafedha nasilaha toka serikali zaMarekani,China,Afrika Kusini,Ivory Coast,Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (wakati huo ikijulikana kamaZaire),Moroko, n.k. Serikali ya Angola ilikuwa ikipata misaada tokaUrusi,Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani,Kuba, naNicaragua.

Tarehe22 Machi2002, Jonas Savimbi aliuawa vitani. Muda mfupi baadaye UNITA na MPLA zilikubaliana kusimamisha mapigano. UNITA ilichukua nafasi ya chama cha upinzani. Hata hivyo taratibu za kidemokrasia zilichelewa hadichaguzi za miaka2008 na2012 na toleo la katiba mpya la mwaka2010.

Demografia

Makabila ya Angola mwaka 1970.
Mwanamke wa Angola pamoja nawatoto nje yakliniki.

Sensa ya mwaka2014 ilihesabu watu 24,383,301 na kufikia mwaka2016 walikuwa 25,789,024.

Kabila

Wakazi wengi ni Waafrika, hasa wa makabila yaWaovimbundu (37%),Waambundu (23%) naWakongo (13%). Machotara ni 2%,Wachina 1,6% naWazungu 1%.

Lugha

Ingawalugha za Kibantu zinaongoza, na 6 kati yake zina hadhi yalugha ya taifa,lugha rasmi niKireno.

Dini

Cathedral yaArchdiocese ya Luanda

Upande wadini, inakadiriwa kuwa zaidi yanusu niWakatoliki narobo niWaprotestanti wamadhehebu mia tofauti.

Tazama pia

Marejeo

    Viungo vya nje

    WikiMedia Commons
    WikiMedia Commons
    Wikimedia Commons ina media kuhusu:

    Serikali

    Habari

    Maoni

    Radio na Muziki

    Maelekezo

    Utalii

    Mambo mengine


    Nchi zaAfrikaBara la Afrika
    Afrika ya Kati (Jamhuri ya) |Afrika Kusini |Algeria |Angola |Benin |Botswana |Burkina Faso |Burundi |Cabo Verde |Chad |Cote d'Ivoire |Eritrea |Eswatini |Ethiopia |Gabon |Gambia |Ghana |Guinea |Guinea Bisau |Guinea ya Ikweta |Jibuti |Kamerun |Kenya |Komori |Kongo (Jamhuri ya) |Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) |Lesotho |Liberia |Libya |Madagaska |Malawi |Mali |Misri |Morisi (Visiwa vya) |Mauritania |Moroko |Msumbiji |Namibia |Niger |Nigeria |Rwanda |Sahara ya Magharibi |Sao Tome na Principe |Senegal |Shelisheli |Sierra Leone |Somalia |Sudan |Sudan Kusini |Tanzania |Togo |Tunisia |Uganda |Zambia |Zimbabwe
    Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje yaAfrika
    Hispania:Kanari·Ceuta·Melilla |Italia:Pantelleria·Pelagie |Ufaransa:Mayotte·Réunion |Uingereza:·St. Helena·Diego Garcia |Ureno:Madeira
    Makala hii kuhusu maeneo yaAfrika bado nimbegu.
    Je unajua kitu kuhusuAngola kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
    Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
    Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
    Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Angola&oldid=1473245"
    Jamii:
    Jamii iliofichwa:

    [8]ページ先頭

    ©2009-2026 Movatter.jp