Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Almere

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mji wa Almere

Almere ni mji na manispaa ya mkoa waFlevoland, nchiniUholanzi. Mji umepakana naLelystad naZeewolde. Ndani ya manispaa ya Almere kuna wilaya yaAlmere Stad,Almere Haven,Almere Buiten,Almere Hout,Almere Poort (bado inajengwa) naAlmere Pampus (ipo katika hatua ya usanifu).

Almere ni mji mdogo nchini Uholanzi: nyumba ya kwanza ilimalizika mnamo 1976, na Almere ikawa manispaa mnamo 1984. Ni manispaa kubwa sana katikaFlevoland ikiwa na idadi ya wakazi takriban 184,405 (7 Julai 2008)[1], na mji wa 8 kwa ukubwa nchiniUholanzi[2]. Mnamo mwezi wa Oktoba 2007, halmashauri ya jiji ya Almere imekubaliana na serikali kupanua mji na kufikia kuwa na wakazi wapatao 350,000 hadi ifikapo mwaka wa 2030.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Mipango ya awali yaIJsselmeerpolders aliona ardhi ikitumika kwa ajili ya kilimo. Hata hivyo, baada yaVita Kuu ya Pili ya Dunia ujenzi wa majumba ulihitajika kwa ukuzaji haraka wa idadi ya watu mjiniAmsterdam na miji miwili ilipangwa katika sehemu za ardhi ya Oostelijk Flevoland na Zuidelijk Flevoland. Mji katika eneo la Oostelijk Flevoland likawaLelystad. Mji katika eneo la Zuidelijk Flevoland uliendelea kuitaZuidweststad (Kiswahili: Mji wa Kusini Magharibi) katika hatua za mwanzoni, lakini katika miaka ya 1970 mji ukawaAlmere, umepewa jina baada ya jina la zama za kati laZuiderzee. Nyumba ya kwanza mjini Almere ilimalizwa mnamo 1976. Kwa kipind hicho mji bado ulikuwa ukimilikiwa naOpenbaar Lichaam Zuidelijke IJsselmeerpolders (Z.IJ.P.), ikiwa naLanddrost. Mnamo mwaka wa 1984 Almere ikapata kuwa manispaa rasmi. Awali, Almere ulitazamiwa kama mji wenye vituo kedekede. Wazo hili lilitelekezwa hapo baadaye kwa hisani ya kuwaruhusu majirani kama vile Tussen de Vaarten kujenga makazi yao mjini hapa. Pia kuna tofauti kadhaa katika mtindo wa ujenzi wa majumba ya sasa na yale ya zamani katika baadhi ya maeneo ya mji huu. Mpango wa ujenzi wa majumba ya mjini Almere kunako miaka ya 1970s ulikuwa wa pamoja na uliangalia sana hadhi ya usawa kijamii. Hata hivyo, kuanzia miaka ya 1990 majumba ya hali ya juu yalijengwa huku yakipishana na mfumo wa ujenzi (mfano kwenyeRegenboogbuurt).

Demografia

[hariri |hariri chanzo]
Theater "Schouwburg Almere"
 Almere HavenAlmere StadAlmere BuitenAlmere HoutAlmere PoortAlmere PampusAlmere in total
1970      52
1975      47
19806596     6632
198521410172401559   40297
1990223553702411499   71087
1995223765881622740564  104496
20002223783934352901336  142797
200522590103560473581366  175008
200722507105261517511345134 180998

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  1. (Kiholanzi)CBS Statline. Retrieved on 2008-06-09.
  2. (Kiholanzi)CBS Statline - Bevolking; ontwikkeling in gemeenten met 100 000 of meer inwoners. Retrieved on 2008-06-09.

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Almere&oldid=1366813"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp