Sehemu kubwa ya nchi nijangwa,Sahara iko upande wa kusini.Asilimia 20 za eneo la Aljeria upande wakaskazini ni makao kwa karibu wakazi wote. Maeneo haya nipwani yaMediteranea namilima ya Atlas. Atlas inapanda hadikimo chamita 2,308 juu yaUB.
Sahara inaanza kusini kwa Atlas na kanda yenyenyasi chache, halafu inafuata eneo la matuta yamchanga pasipomimea yote. Kusini kwake tena ninyanda za juu ambazo ni hasa maeneo yamiamba mitupu.
Kusini kabisa kuna milima kamaTassili n'Ajjer naAhaggar inayopanda hadi mita 2,918 na kuwa kama visiwa vya uoto katika jangwa.
Mito ya kudumu iko kaskazini tu, sehemu za pwani.Mabonde ya mito ya ndani ni makavu, isipokuwa baada yamvua mito mikali inajitokeza kwa masaa kadhaa.
Kanda la kaskazini linahali ya hewa inayoathiriwa na Bahari ya Mediteranea. Hukohalijoto kwenyemweziAgosti ni 25°C na 12 °C wakati waJanuari.
Kwenye sehemu za juu kunabaridi na hatabarafu kwenyemajira ya Januari lakinijoto ni kali zaidi wakati wa Julai/Agosti.
Kusini ya Atlas inaanza hali ya hewa ya jangwani; halijoto inaweza kucheza zaidi ya 20 °C katika siku moja. Wakati wa joto halijoto inapita 40 °C lakini wakati wa baridi halijoto inashuka chini ya °C kwenye saa zausiku.
Mvua ni haba mno: kuna miaka mfululizo bilatone hata moja. Katika milima ya Ahaggar kunausimbishaji kidogo kutokana naukungu, kwa hiyomiti kadhaa namimea mingine iko.
Kuanzia mwaka642 vikosi vya Waislamu Waarabu kutokaMisri walishambulia eneo la Afrika ya Kaskazini. Mwanzoni hawakufaulu kuwashinda Wabizanti lakini, baada yauhamisho wa serikali ya makhalifa kutokaMedina kwendaDameski,Waumawiya walikazajitihada huko Afrika ya kaskazini.
Mwaka670jeshi kubwa la Waarabu likaunda mji waKairuan kusini yaTunis ya leo na mji huu ulikuwakitovu cha uenezaji. Walipoenea katika Aljeria ya leo walirudishwa na WaberberWakristo kwa msaada wa Wabizanti lakini jeshi lililofuata lilishinda na kufikia mwaka711 Afrika ya kaskazini yote (maana yake nchi za leo za Tunisia, Aljeria na Moroko) zilikuwa chini ya utawala wa Waarabu. Hapo sehemu kubwa ya Waberber walifanya haraka kujiunga na Uislamu wakasaidiana na Waarabu.
Matokeo hayo yalikuwa chanzo cha mabadiliko makubwa ya kudumu, maana yake upanuzi wa lugha ya Kiarabu kati ya wananchi na uenezaji wa Uislamu.