Makao makuu ya kampuni ya Alibaba Group huko Hangzhou
Alibaba Group Holding Limited (pia hujulikana kamaAlibaba) nikampuni yateknolojia ya kimataifa yenye makao makuu yake nchiniChina iliyobobea katikabiashara ya mtandaoni na teknolojia .
Ilianzishwa mnamo28 Juni1999 hukoHangzhou,Zhejiang kampuni hiyo hutoa huduma za mauzo ya watumiaji kwa watumiaji (C2C), biashara kwa watumiaji (B2C), na biashara kwa biashara (B2B) kupitia lango zawavuti, pia hutoa huduma za malipo ya kielektroniki, injini za utaftaji wa ununuzi, na huduma zakompyuta ya wingu. Inamiliki na kuendesha matawi mengi ya kampuni ulimwenguni kote katika sekta nyingi za biashara.[1]
Mnamo19 Septemba2014, uwekezaji wa shea wa Alibaba (IPO) kwenye Soko lahisa laNew York ulikusanyadola za Kimarekani bilioni 25, na kuipa kampuni hiyo thamani ya soko la dola za Kimarekani bilioni 231. Hadi sasa IPO ni kubwa zaidi katikahistoria duniani.[2] Ni mojawapo ya mashirika 10 yenye thamani zaidi[3] na imetajwa kuwa kampuni ya 31 kwa ukubwa duniani kwenye orodha yaForbes Global 2000 mwaka2020.[4] MnamoJanuari2018, Alibaba ilikuwa kampuni ya pili katika bara laAsia kwa kuwa na thamani ya dola Kimarekani bilioni 500, baada ya mshindani wake kampuni ya Tencent.[5]
Makala hii kuhusu mambo yauchumi bado nimbegu. Je, unajua kitu kuhusuAlibaba Group kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.