Kaulimbiu ya taifa:لا إله إلا الله، محمد رسول الله (Shahada) Lā ilāhā illā-llāhu; muhammadun rasūlu-llāhi ("Hakuna mungu ilaAllah;Muhammad ni mtume wa Allah")
Afghanistan ni nchi bilapwani kwenyebahari yoyote. Sehemu kubwa ya eneo lake lenyekm² 652,090 nimilima.Asilimia 90 za nchi ikomita 600 au zaidi juu yaUB ikiendelea kupanda hadi mita 7,485 kwenye ncha yamlima Noshak. Safu za milima kubwa niHindu Kush naPamir.
Katika kaskazini na kusini magharibi kuna maeneo ya tambarare yenye tabia yajangwa. Maeneo makubwa niyabisi na nusu jangwa au jangwa. Sehemu za milima zinapokeamvua natheluji, lakinimito mingi inayoanzia huko inapelekamaji yake nje ya nchi, kwenda Iran, Pakistan na Turkmenistan.
Kabla yakarne ya 19 nchi yote au sehemu mbalimbali zilikuwa chini yamilki jirani, hata kama sehemu za eneo la Afghanistan zilijitegemea chini ya watawala wadogo. Kwa vipindi virefu vyahistoria Afghanistan ilikuwa sehemu yamilki zaUajemi (Iran).
Afghanistan kama nchi ya pekee ilianza kutokea katikakarne ya 18, watawala wa kieneo walipojiondoa katika himaya ya Uajemi.
Nchi ilifaulu kutunzauhuru wake kutokana na mashindano yaUingereza naUrusi pamoja na nguvu na ukali wa wapiganaji kutokamakabila yake. Watawala wa kwanza waliofaulu kuunganisha sehemu nyingi za nchi chini yamamlaka yao walitawala kamaEmir, na tangumwaka1926 kwacheo chamfalme.
Mnamo Disemba1979Umoja wa Kisovyeti iliamua kuingilia kati ikavamia nchi kwa shabaha ya kuokoa utawala wa Wakomunisti, lakini ukapaswa kujiondoa tena mwaka1989.
Vita vya wenyewe kwa wenyewe vilifuata kati ya vikundi vya wapinzani ambako nchi jirani yaPakistan ilikuwa na athira kubwa kwa kutumasilaha napesa. Nchi ilikuwa tena na kipindi kifupi chaserikali ya kitaifa, lakini vita vya wenyewe kwa wenyewe viliendelea katika sehemu za nchi.
Mateso ya vita hivyo yalihamasishawalimu nawanafunzi wamadrasa (shule zaKiislamu) kuchukua silaha dhidi ya migambo mbalimbali na kuwashinda wakijulikana kwa jina laTaliban (jina linamaanisha wanafunzi wa madrasa). Taliban walifaulu kutekaKabul kwa msaada kutokaSaudia na Pakistan mwaka1996. Walitangaza Emirati ya Kiislamu ya Afghanistan wakanzisha utawala uliotumia mafundisho makali yasharia ya Kiislamu. Utawala wao ulikuwa maarufu kwa kuzuia wanawake wasishiriki katikamaisha ya hadharani, kuwalazimisha kuvaaburka, kufunga shule za wasichana, kukatazakazi kwa wanawake nje yanyumba zao tena matumizi yaadhabu kali kama kukatamkono wamwizi na kumwuamzinzi kwa kumpigamawe.
Hali ya vita iliendelea ndani ya Afghanistan katika vita vya Marekani naNATO2001-2014. Tangu Disemba 2014 nchi za NATO zilitangaza ya kwamba wamemaliza kushiriki mapigano na kuondoa sehemu kubwa yawanajeshi kutoka Afghanistan. Vikosi vya NATO vimebakizwa kwa shabaha ya kusaidia jeshi la kitaifa.
Mnamo mwaka2020 Marekani ilipatana na Taliban kwamba Marekani ingeondoaaskari wote kutoka Afghanistan katika mwaka 2021. Taliban waliahidi kutoshambulia wanajeshi wa Marekani lakini waliongeza mashambulio yao dhidi ya jeshi la serikali.
Baada ya kuondoka kwa wanajeshi wa NATO na idadi kubwa ya Wamarekani, Taliban walianza kuvamia maeneo mengi ilhali nguvu ya jeshi la kitaifa liliporomoka. Mnamo15 Agosti 2021, rais wa Afghanistan aliondoka nchini na Taliban waliteka tena Kabul.
Baada ya kutwaa Kabul, wasemaji wa Taliban walitangaza kwamba wanataka kufuatasiasa tofauti kiasi na ile ya zamani. Wasemaji walidai kwamba wataruhusu wanawake kufanya kazi na wasichana kusoma, kama wanakubali kuvaahijabu. Walitangaza pia kwamba watasamehe wananchi wote waliowahi kupigana nao. Hata hivyo, Waafghanistan wengi walijaribu kukimbia nchi kwa njia mbalimbali.
Mwisho wa Agosti 2021, Taliban walidhibiti nchi yote isipokuwa jimbo laPanjshir, ambapo wapinzani walijipanga chini ya makamu wa rais aliyejitangaza kuwarais kufuatana nakatiba ya jamhuri.
Watu
Mwaka2015 wakazi walikadiriwa kuwa 32,564,342, wakiwemo wakimbizimilioni 2.5 wanaoishi Pakistan na Iran.
Kwa kuwa nchi iko kwenye njia zinazounganisha maeneo mbalimbali ya Asia, wakazi hao ni mchanganyiko mkuuːkabila kubwa ni laWapashtuni (42%), halafu kunaWatajiki (27%),Wauzbeki (9%),Wahazara (8%) n.k.
1. Nchi ina maeneo katikaAsia naUlaya. 2. Nchi ikoAsia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi zaUlaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.
Makala hii kuhusu maeneo yaAsia bado nimbegu. Je unajua kitu kuhusuAfghanistan kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.