Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Abraham Lincoln

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Abraham Lincoln


Muda wa Utawala
Machi 4, 1861  Aprili 15, 1865
Makamu wa RaisHannibal Hamlin (1861–1865)
Andrew Johnson (Machi–Apr. 1865)
mtanguliziJames Buchanan
aliyemfuataAndrew Johnson

tarehe ya kuzaliwa(1809-02-12)Februari 12, 1809
Kentucky,Marekani
tarehe ya kufa15 Aprili 1865 (umri 56)
Washington, D.C.,Marekani
mahali pa kuzikiwaLincoln Tomb
chamaWhig (Kabla ya 1854)
Republican (1854–1864)
National Union (1864–1865)
ndoaMary Todd Lincoln (m. 1842) «start: (1842-11-04)»"Marriage: Mary Todd Lincoln to Abraham Lincoln"Location:(linkback://sw.wikipedia.org/wiki/Abraham_Lincoln)
watotoRobert Todd Lincoln
Edward Baker Lincoln
William Wallace Lincoln
Tad Lincoln
signature
Uuaji wa Lincoln.

Abraham Lincoln (12 Februari180915 Aprili1865) alikuwaRaiswa 16 waMarekani kuanziamwaka wa1861 hadi1865.

Alikuwa naKaimu Rais wawili: kwanzaHannibal Hamlin, halafuAndrew Johnson aliyemfuata kama Rais, Lincoln alipouawa.

Lincoln amejulikana kamarais wa upande wakaskazini katikavita vya wenyewe kwa wenyewe vya Marekani kati yamajimbo ya kaskazini dhidi yaShirikisho la Madola ya Amerika lakusini.

Kwa hiyo hukumbukwa kama rais aliyeleta mwisho wautumwa, yaaniuhuru kwawatumwa wote wa Marekani na kuunganishataifa tena.

Juhudi zake zilimgharimuuhai.

Lincoln na kufutwa kwa utumwa

[hariri |hariri chanzo]

Lincoln aliingia katikasiasa alipokuwawakili hukoSpringfield, Illinois;mwaka1846 alichaguliwambunge wa kitaifa katikaNyumba ya Wawakilishi kwa kipindi kimoja. Mwaka1849 alirudi kwafamilia yake nakazi ya uwakili. Mwaka1856 aliingia tena kwenye siasa alipoona upanuzi wa nguvu ya watetezi wa utumwa katika majimbo ya kusini ya Marekani. Aliundatawi la Illinois yaRepublican Party akateuliwa kuwa mgombea wa urais akachaguliwarais wa Marekani kwenye Desemba1860.

Lincoln alipinga utumwa lakini kwaasili hakuwa mpinzani mkali; aliona kwamba utumwa uliwahi kukubaliwa katikakatiba ya Marekani tangu mwanzo lakini aliona hali hiyo iendelee katika majimbo ya kusini tu yaliyokuwa sehemu za Marekani tangu mwanzo ilhali majimbo ya kaskazini yaliukataa. Alipinga upanuzi wa utumwa katika majimbo mapya yaliyoendelea kuundwa wakatiMuungano wa Madola ya Amerika ulipanua eneo lake upande wamagharibi na kuelekeautawala juu ya nchi yote kati yaKanada naMeksiko.

Alipinga hatua yamajimbo ya kusini kujitenga na baada ya mashambulio dhidi ya vituo vya kijeshi vyaMuungano aliamua kuchukua hatua za kijeshi ili kurudisha majimbo yaliyoasi. Mwanzoni mwavita alitangaza nia yake haikuwa kumaliza utumwa kusini; lakini baada ya vita kuendelea miaka miwili alikuwa tayari kuchuka hatua kali zaidi.

Mwaka1862 alitiasahihi tangazo la Bunge la Muungano kuwa watumwa wote waliomilikiwa naaskari waliopiga vita dhidi ya Muungano wakamatwe na kutangazwa huru. Mwisho wa 1862 Lincoln mwenyewe alitoaamri ya kutangazauhuru wa watumwa wote katika majimbo yote yaliyotumiasilaha dhidi ya Muungano. Alikubali pia kuajiri watumwa kuwawanajeshi kama wamekimbia kutoka upande wa kusini na kujitolea. Hakufuta kabisa utumwa kwa sababu bado kulikuwa na majimbo machache yenye utumwa yaliyobaki katika Muungano. Baada ya mwisho wa vita Lincoln alipata kibali cha bunge cha kufuta utumwa kabisa katika maeneo yote ya Marekani.

1 George Washington ·2 John Adams ·3 Thomas Jefferson ·4 James Madison ·5 James Monroe ·6 John Quincy Adams ·7 Andrew Jackson ·8 Martin Van Buren ·9 William Henry Harrison ·10 John Tyler ·11 James K. Polk ·12 Zachary Taylor ·13 Millard Fillmore ·14 Franklin Pierce ·15 James Buchanan ·16 Abraham Lincoln ·17 Andrew Johnson ·18 Ulysses S. Grant ·19 Rutherford B. Hayes ·20 James A. Garfield ·21 Chester Arthur ·22 Grover Cleveland ·23 Benjamin Harrison ·24 Grover Cleveland ·25 William McKinley ·26 Theodore Roosevelt ·27 William Howard Taft ·28 Woodrow Wilson ·29 Warren G. Harding ·30 Calvin Coolidge ·31 Herbert Hoover ·32 Franklin D. Roosevelt ·33 Harry S. Truman ·34 Dwight D. Eisenhower ·35 John F. Kennedy ·36 Lyndon B. Johnson ·37 Richard Nixon ·38 Gerald Ford ·39 Jimmy Carter ·40 Ronald Reagan ·41 George H. W. Bush ·42 Bill Clinton ·43 George W. Bush ·44 Barack Obama ·45 Donald Trump ·46 Joe Biden ·47 Donald Trump
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Abraham_Lincoln&oldid=1116692"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2026 Movatter.jp